TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, September 20, 2013

VIONGOZI WA TAARABU, MNAWAENZI VIPI WASANII WANAOKUFA?

 Tokea kifo cha wasanii 13 wa 5 Star mpaka sasa ni wengi wametangulia mbele ya haki tukiamua kuwataja mmoja mmoja, lakini swali linakuja nini wamefanya hata tu kuwaenzi wasanii waliofariki hata kufanya kisomo cha pamoja kuwarehemu tu!. 

Mimi kama mwandishi wa taarabuzetu.blogspot.com na mdau mkubwa wa mziki huu wa mwambao, Katika kumbukumbu zangu 5 Star walifanya hitma ya pamoja iliyofanyika katika ukumbi wa PTA mtoni kwa azizi ally lakini baada hapo hakuna kilicho endelea tena, wakati mwingine huwa napatwa na maswali kwani katika tasnia ya taarabu hakuna chama kinachotetea masirahi na haki za wasanii? na kama kipo kinafanya kazi gani? ni aibu sana.

Viongozi wa Bendi za Taarabu ni vyema kama mngekaa pamoja mkajipanga kama timu moja mkaelewana namna ya kuweza kundeleza bendi pamoja na mambo mengine ya muhimu.

2 comments:

Anonymous said...

Hili ni la msingi sana na nimekua nikilipigia kelele kwa nguvu zangu zote ila watu wa Taarab ubinapsi umezidi sana na majungu na ufahamu finyu ndio tatizo

Anonymous said...

Siku zote umoja huwa muhimu sana, sasa hawa watu wa Taarabu wao wanajiona akiwa peke ya ni vizuri zaidi na akimshirikisha mwenzake anaona kama atakuwa amemtoa, yaani kifupi ni Ubinafsi na Majungu mengi.
Kamwe haitatokea wameungana...

Post a Comment