TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Sunday, August 25, 2013

AHMED MGENI UPO WAPI?.TUMEMISS BURUDANI ZAKO!

Muimbaji wa Zanzibar njema Modern Taarab Ahmed Mgeni amepotea kwa kipindi kirefu haonekani kwenye maukumbi wala mazoezini. 

Mtandao huu umekuwa ukipigiwa simu na wadau mashabiki na wapenzi wanaompenda Ahmed Mgeni kutaka kujua huyu mtu yupo wapi kwa sasa.

Mtandao wa taarabuzetu.blogspot.com ulifanya uchunguzi wake na kugundua kwamba Ahmed Mgeni alikwenda Uarabuni lakini hakukaa sana akaanza kuugua ndipo aliporudishwa Tanzania na kwenda moja kwa moja Visiwani Zanzibar kwa matibabu zaidi. 

Hata hivyo alipopigiwa simu mkurugenzi wake hakupatikana kwenye simu lakini tutaendelea kumtafuta ili aweze kutueleza mambo mengine hasa kuhusu Ahmed Mgeni..

0 comments:

Post a Comment