TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, August 22, 2013

HASSAN ZUMO AAMUA KUTOKA KIVYAKE...

Hassan Zumo.
 Muimbaji wa kutegemewa wa bendi ya Supershine Modern Taarabu Hassan Zumo, anakuja na wimbo uitwao "Niacheni Nipagawe" nje ya bendi yake. 

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Zumo alisema wimbo huo anategemea utamnyanyua na kumuweka juu zaidi kulingana na mashairi, muziki na ujumbe husika uliopo katika wimbo huo, katika wimbo huo kinanda kimepigwa nae Omary Kisila solo gitaa limepigwa na Ramadhan Kisolo na Besi gitaa kapiga Side James. 

Zumo amewaomba wapenzi kumpa sapoti ili aweze kufikia malengo aliyojiwekea katika suala zima la sanaa.

0 comments:

Post a Comment