TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, August 15, 2013

G5 MODERN TAARABU, KUANZA "BONANZA" KILA JUMAPILI...

Baadhi ya wasanii wa G5 Modern Taarabu.
 Bendi ya G5 Modern Taarabu itakuwa ikifanya onyesho la Bonanza kila Jumapili, na itaanza jumapili hii tarehe 18/8/2013.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Mkurugenzi wa bendi hiyo Hamisi Slim alisema kwamba katika bonanza hilo kutakuwa na vikundi mbalimbali vya burudani vitakavyokuwa vikishirikiana nao, Hamis alivitaja vikundi hivyowakiwemo kundi la Kanga moja na Mavampaya watoto wa TMK, Vile vile Dogo Asley ataongoza kundi la Mkubwa na wanawe, kama hiyo haitoshi wanafikilia kuwaongeza kundi la Baikoko na Msagasumu ili kunogesha zaidi Bonanza hilo.

Mkurugenzi Hamisi Slim alisema Bonanza hilo litakuwa likifanyika kila Jumapili katika ukumbi wa IKWETA GRILL Mtoni kwa Azizi Ally.

Wapenzi wa G5 wameombwa kuhudhulia ili kupata burudani kila Jumapili kabla ya kuingia makazini Jumatatu, Pata burudani kibao na G5 Modern Taarabu!

0 comments:

Post a Comment