TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Wednesday, August 14, 2013

SUPERSHINE MODERN TAARABU KUTAMBULISHA NYIMBO MPYA MAX BAR ILALA.

Baadhi ya wasanii wa Supershine
 Bendi ya Supershine Modern Taarabu baada ya kutoka katika Shangwe za sikukuu ya IDD, leo siku ya Jumatano wanatarajia kuporomosha burudani ya nguvu katika ukumbi wa Max Bar uliopo Ilala. 

Akizungumza na mtandao makini wa taarabuzetu.blogspot.com Msanii wa bendi hiyo ambae pia ni MC Hassan Zumo aliwaomba wapenzi wa bendi hiyo kujitokeza kwa wingi kuja kushuhudia mambo mazuri ambayo wameyaandaa kwa muda wote wa kipindi cha Ramadhani. 

Supershine Modern Taarabu huwa wanatoa burudani zao katika kumbi za Max Bar Ilala kila Jumatano na Lango la jiji kila Alhamisi, wapenzi wote mnakaribishwa.

0 comments:

Post a Comment