TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Sunday, August 18, 2013

IFIKE WAKATI WASANII WA TAARABU WASAINI MIKATABA YAO MBELE YA WANASHERIA...

 Muziki wa taarabu umekuwa ukipata mafanikio kila kukicha na kufanya hata makampuni makubwa hapa Tanzania kuanza kutangaza bidhaa zao kupitia vipindi vya muziki huo katika Redio na televisheni mbalimbali, Lakini asilimia kubwa ya wasanii wa muziki huu wamekuwa hawajui haki zao au wao pia kukiuka mikataba ambayo wamekuwa wakiwekeana kiholela na wamiliki mbalimbali wa mabendi husika. 

Mfano Msaani kama Bi mwanahawa ally! amekuwa akizitumikia bendi zaidi ya mbili ama tatu kwa kurekodi nyimbo mpya au kufanya Show katika bendi zote hizo.

Sasa balaa ni pale bendi hizo zote zinapoingiza albamu zake sokoni, utakuta katika kila albamu moja kuna nyimbo mpya kaimba Bi Mwanahawa Ally, sasa hapa kwanza mashabiki wanashindwa kujua huyu mama yupo bendi ipi moja wapo kati ya hizo?.

Ukirudi upande wa pili wakulaumiwa ni viongozi wa bendi hizo, ni kwanini wanamuimbisha Bi mkubwa huyo wakati hawana mkataba nae?. 

Imefika wakati sasa kwa viongozi wa Taarabu na wasanii kwa ujumla kuzijua haki zao kisheria ili kila mmoja afanye kazi kulingana na mkataba unavyosema. 

Hii tabia ya kuandikishiana mkataba kama mnapeana maji ya kunywa imepitwa na wakati sasa. TUBADILIKE

0 comments:

Post a Comment