TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Tuesday, August 13, 2013

TETESI:- RAMADHAN KISOLO ATAKIWA NA BENDI ZAIDI YA TATU...

Ramadhan Kisolo "Mwana Malui", Mpiga Solo wa Mashauzi Classic.
 Katika kile kinachooneka ni kutaka kuidhoofisha bendi ya Mashauzi Classic, Zaidi ya Bendi tatu za taarabu nchini zimeanza kumuwania kwa udi na uvumba Mpiga solo maarufu wa bendi hiyo aitwae Ramadhan Kisolo "Mwana Malui", 

Akizungumza na msanii huyo mwandishi wa habari hizi alitaka kujua je tetesi hizi zinaukweli wowote?, Kisolo alisema "mimi ni msanii wa Mashauzi Classic na sina mpango wa kuhama bendi hii kwani mkurugenzi wangu Isha amekuwa akinitimizia kila kitu hivyo nawaambia hao wanaozusha habari hizi kuacha kuniharibia kwa Bosi wangu".

0 comments:

Post a Comment