TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, August 16, 2013

ALLY STAR AMPONDA THABIT ABDUL...!!

Ally Hemed Star wa T.O.T.
 Muimbaji mkongwe wa T.O.T. Taarabu Ally Star amemponda Thabit Abdul kwa kujiita yeye ndo muanzilishi wa mtindo wa TARADANCE.

Ameshangazwa na habari iliyoandikwa na mtandao huu kwamba Thabit Abdul yeye ndio muanzilishi wa taradance hapa nchini kitu ambacho sio kweli kabisa. na kusema kwamba muanzilishi wa Taradance hapa nchini ni yeye. 

Aliyasema hayo wakati alipopiga simu ofisini kwetu na kusema kwamba huyo Thabit asijisifie kwa kitu ambacho hajakiunda yeye wala hana uzoefu nacho zaidi ya kukopi tu!, mimi nimetoa wimbo wenye miondoko ya Taradance uitwao MVUVI KINDA kabla yake yeye!, hivyo yeye kakopi toka kwangu na kujitangazia kuwa muanzilishi, tafuta hiyo nyimbo usikiliza kaka kisha uniambie!.

0 comments:

Post a Comment