TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Sunday, August 25, 2013

HASSAN VOCHA NA HASNA MASAUTI WA G5 KUTIMKIA BENDI NYINGINE...

Hasna Juma (Masauti) na Hassan Vocha.
 Hassan Vocha na msanii mwenzake wa G5 Modern Taarabu Hasna Masauti kutimkia katika bendi ya King's Modern Taarabu.

Wasanii chipukizi Hassan Vocha na Hasna Masauti wa bendi ya G5 Modern Taarabu wanawindwa kwa udi na uvumba na bendi inayokuja kwa kasi ya Kings Modern Taarabu ya jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mtandao wa taarabuzetu.blogspot.com Rais wa Kings Mrisho Rajabu alisema wamegundua uwezo mkubwa walionao vijana hao na wao kama Kings wanahisi itakuwa vyema zaidi kama watawanunua ili kuja kuipa nguvu bendi ya Kings. 

Alipopigiwa simu Hassan Vocha alisema ni kweli amepigiwa simu na kiongozi huyo ila hawajafikia muafaka bado, mazungumzo yanaendelea!.

0 comments:

Post a Comment