TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, August 22, 2013

HASHIM SAIDI:- SIJAMLENGA YEYOTE...

Hashim Said Igwee (Mzee wa Majanga).
 Sijamuimba mtu yeyote katika wimbo wangu nilioutoa hivi karibuni wa Bonge la Bwana naomba nisieleweke vibaya.

Kiongozi wa wasanii katika bendi ya Mashauzi Classic na muimbaji wakutumainiwa Hashim Saidi au mzee wa Majanga amekuwa akilalamikiwa kwamba wimbo wake wa Bonge la Bwana amemuimba mke wake wa zamani, jambo ambalo mwenyewe amekanusha. 

Akizungumza na mtandao makini wa taarabuzetu.blogspot.com Hashim Saidi alisema kwamba kumuimba mtu ulieachana nae inaonyesha kama bado unamuhitaji jambo ambalo kwangu halipo na wala sithubutu, nilichokitapika kamwe siwezi kukila tena ni sawa na kutia ulimi puani jambo lisilo wezekana!. 

Huo ni wimbo tu, sikumlenga yeyote

1 comments:

Unknown said...

mmmmh... sijasikia mwivi kuiba akanadi ameiba.

Post a Comment