TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Saturday, August 31, 2013

TETESI:- MWINJUMA MUUMIN AJIUNGA NA G5 MODERN TAARABU...

 Kuna tetesi kuwa Kiongozi wa Victoria Sounds - Mwinjuma Muumini amejiunga na G5 Modern.
 
Mwanamuziki nguli na mkongwe katika ulimwengu wa dansi nchini Mwinjuma Muumin au Kocha wa Dunia inasemekana amejiunga na bendi ya taarabu ya G5 Modern Taarabu inayomilikiwa na Hamisi Slim.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wadau wa taarabu wa eneo la Mtoni kwa Azizi Ally ambapo bendi ya G5 hufanya maonesho yake, wamesema kwamba wamekuwa wakimshuhudia Muumin akihudhuria katika maonyesho ya bendi hiyo usiku wa manane jambo walilo tafsiri kwamba Muumin amejiunga na bendi hiyo.

Akizungumza na mtandao huu mkurugenzi wa bendi hiyo Hamisi Slim aliweka wazi kuwa, hakuna kitu kama hicho, isipokuwa Muumin ni rafiki yake wa muda mrefu hivyo huwa anamtembelea tu!.

0 comments:

Post a Comment