TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Saturday, August 24, 2013

MAPENZI YA FACEBOOK...!!!

Hemedi Omary
 Mapenzi ya Facebook kutambulishwa rasmi Jumatatu...!! 

Wimbo mpya wa Muimbaji Hemedi Omary "Mapenzi ya Facebook" ambao umerekodiwa jana katika Studio ya BMD RECORD Mbagala jijini Dar umekamilika na utatambulishwa rasmi siku ya Jumatatu katika radio mbalimbali, pia utaipata katika mtandao huu wa taarabuzetu.

Hemed Omary alisema kwamba anamshukuru mungu kwa kumuwezesha kurekodi wimbo huo na wadau wasubiri kusikia kazi nzuri toka kwake. 

Katika wimbo huo kinanda kimepigwa na Mzaka Nundu, 
Gitaa la Solo limepigwa Jongo na gitaa la besi limechalazwa nae Hamadi besi. 

Hemdi Omary ni msaani wa bendi ya TOT TAARABU pia ni mtunzi mzuri wa nyimbo za Taarabu. 

Nyimbo alizowahi kutunga Hemed ni "Tugawane ustaarabu" ya Isha, "Top in Town" ya Khadija kopa na zingine nyingi.

0 comments:

Post a Comment