TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Sunday, August 25, 2013

ZANZIBAR STARS KURUDI TENA KWA NGUVU MPYA...!!

Baadhi ya wasanii wa Zanzibar Stars.
Nipo mbioni tena kuirudisha Zanzibar Stars...
Hayo ni maneno ya muanzilishi wa bendi ya Zanzibar Star's, Bakary Shomari wa visiwani Zanzibar.

Akizungumza kwa njia ya simu toka visiwani humo Bakari Shomari alisema kwa sasa yupo tiyari kabisa kuirudisha kwenye game bendi yake hiyo kongwe ya Zanzibar Stars, kinachompa moyo zaidi wa kuanzisha tena kundi hilo ni kuona baadhi ya waanzilishi wenzake kama Bi Sihaba Juma na Rukia Ramadhan wakisema kwamba wapo tayari kuungana nae pindi bendi itakapokuwa tayari. 

Kipindi cha hivi karibuni kuna wajanja flani flani wamekuwa wakijikusanya na kufanya show kwa jina la Zanzibar Star's feki na kupiga hela nzuri tu kutokana na umaalufu wa bendi hiyo!

Bwana  Bakari Shomari alisema pindi atakapokuwa amekamilisha mambo yake, ataizindua rasmi ili wapenzi wote wajue kuwa Zanzibar Star ipo hewani na wala si ile feki tena.

0 comments:

Post a Comment