TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Saturday, August 17, 2013

TETESI:- SALEHE MUSSA WA SUPERSHINE ATIMKIA GUSAGUSA MIN BEND...!!

Salehe Mussa
 Kuna tetesi zimevuma kuwa, mpiga kinanda wa kutumainiwa wa bendi ya Supershine Modern Taarabu "Chuo cha mafunzo" ametimkia kwa wana Gusagusa Min Bend ya hapahapa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mkurugenzi wa Supershine Dr Noh! alisema kwamba yeye hana uhakika kama msanii wake Salehe Mussa amehama bendi, kwani hajamwambia lolote isipokuwa ameshangaa tu kuona Salehe Mussa hajatokea katika show ya pale Max Bar Ilala jumatano na pia hajatokea siku ya alhamisi katika show ya pale Lango la Jiji Magomeni. 

Mwandishi wa taarabuzetu.blogspot aliamua kumtafuta Salehe Mussa kwa namba yake ya simu ya mkononi lakini hakupatikana na mpaka habari hizi zinachapishwa simu yake haipatikani.

Hata hivyo Salehe Mussa ameonekana katika show ya Gusagusa Min Bend akipapasa kinanda kwa raha zake.

0 comments:

Post a Comment