TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Monday, August 26, 2013

HAMMER Q NA SALHA ABDALLAH: TUMEWAKOSEA NINI? SEMENI TUWALIPE...!

Hammer Q na Mkewe Salha.
 Wasaani wawili ambao ni wanandoa Hammer Q wa 5 Stars na Salha Abdallah wa Kings Modern Taarabu hivi karibu walitoa wimbo wenye mahadhi ya mduara na waliuimba pamoja wimbo huo uitwao TUNAPENDANA ni wimbo ambao umekuwa ukifanya vizuri sana katika vituo mbalimbali vya redio, juzi umezua balaa baada ya mtu asie julikana kuanza kusambaza sms kwa watangazaji wa redio kwamba wasiupige wimbo huo, Sms yenyewe hii hapa:- "Asalaam aleykum ulickia Hammer Q na Salha walivyo wakashifu watangazaji? Ucjaribu wala kupiga nyimbo zao ili wakione maana wanajua dunia wanaitawala wao".

Akizungumza na mtandao makini wa taarabuzetu.blogspot.com Hammer Q alisema Unajua ndugu mwandishi, ndoa yangu na mke wangu Salha imekuwa na maadui wengi haijapata tokea! na sijui ni nini tumewakosea!, kama kuna kitu wanatudai waseme tuwalipe!.


Juzi nilikuwa nahojiwa mimi na mke wangu Salha katika kipindi cha ng'aring'ari na Sakina Lyoka Clouds TV. Sasa inasemekana mimi niliwaponda watangazaji wa redio na kuwakashifu kitu ambacho sio kweli kabisa, hata kama kipindi kitarudiwa wataona sikusema jambo lolote baya la kuwatusi wala kuwakashifu, Mungu shahidi! Sasa from no where! mtu anatuma sms kwa watangazaji kwamba mimi na mke wangu tunajidai, tunajiona kama dunia tumeibeba, ni jambo ambalo sio kweli, hii ni katika kuchafuliana majina kwa chuki binafsi tu!.

Yaani ndugu mwandishi hatujui kosa letu, tunafuatiliwa sana kwa kila tunalofanya! naomba nichukue nafasi hii kuwaomba radhi watangazaji wote kama waliumizwa na hayo maneno ya uzushi watusamehe mimi na mke wangu kwani wao tunawategemea sana kucheza kazi zetu na mke wangu!.

Ila waelewe wazi kamwe hatuwezi kuwasema vibaya abadani, tunawapenda sana kwani wao ni watu muhimu sana kwa maendeleo ya sanaa yetu. alimalizia.

Sisi pia tunawaomba watu hao kuacha kuchafu wenzao, kwani mtu anapokosea huambiwa ili ajirekebishe sio kumzunguka na kuanza kumsema au kumzushia kitu ambacho hajakifanya kwa lengo la kumvuruga na kumchonganisha na watu.


Hii hapa ni Msg ya Hammer Q kwa niaba ya Salha pia aliyoitoa katika ukurasa wake wa Facebook:-

1 comments:

Anonymous said...

Ilo nenoo! Itabidi watunge wimbo usemao! Tumewakosea nini Semeni tuwalipe

Post a Comment