TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Wednesday, August 28, 2013

SUPERSHINE MODERN TAARABU, KUMTAMBULISHA MPIGA KINANDA WAO MPYA LEO JUMATANO...

Baadhi ya wasanii wa Supershine Modern Taarabu.


Supershine Modern Taarabu leo Jumatano katika Ukumbi wa Max Bar Ilala watamtambulisha rasmi mpiga kinanda wao mpya Ndage Ndage.

Bendi ya Supershine ambayo kwa sasa imekuwa ndio gumzo la jiji zima la Dar, leo jumatano wanatarajia kufanya utambulisho wa nyimbo zao mpya na pia watamtambulisha rasmi mpiga kinanda wao mpya "Ndage Ndage" aliejiunga nao akitokea Mashauzi Classic. 

Akizungumza na mtandao wa taarabuzetu.blogspot.com Mkurugenzi wa bendi hiyo Dk Noh! alisema kwamba wakazi wa Buguruni, Vingunguti, Tabata, Ilala, Kariakoo na maeneo ya jirani wafike kwa wingi kupata burudani nzuri toka Supershine Taarabu, "Tunawaahidi kutakuwa na burudani nzuri na ya kupendeza, kwa kweli leo ndo mtakubaliana nami kuwa Supershine Modern Taarabu si kama ile ya Zamani, tumejipanga vyema kutoa burudani kwa mashabiki zetu, karibuni sana".

0 comments:

Post a Comment