TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, August 23, 2013

JOKHA KASIM, KAPOTELEA WAPI...??

Jokha Kassim
 Unapolizungumzia Jina la Jokha Kasim katika muziki huu wa taarabu hapa nchini, basi kila mmoja anajua kwamba huyo ni mtu wa aina gani katika tasnia hii. 

Jokha Kasimu amekuwa kimya sana tokea atoe wimbo wa "Domo la udaku" mapema mwaka jana akiwa na kundi zima la T MOTTO mpaka sasa hajulikani yupo wapi na anafanya nini katika tasnia hii. 

Wadau wa taarabu wamekuwa wakipiga simu ofisi kwetu kutaka kujua mpendwa wao yupo bendi gani kwa sasa? kwani hata T MOTTO ambayo alikuwepo haifanyi show yoyote jambo linalotafsriwa na wadau kwamba inawezekana imekufa. 

Jokha kasimu ni msanii anaependwa sana na wapenzi wengi wa Taarabu, mwandishi wa mtandao huu alijaribu kumtafuta katika simu yake ili aweze kuwaeleza mashabiki wake aliko, lakini bila mafanikio simu yake ilikuwa haipatikani, hata hivyo tutamtafuta ili aweze kuelezea ukimya wake ni nini hasa...!!?

0 comments:

Post a Comment