TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Tuesday, August 13, 2013

IDDI TATU... TAARABU YAADIMIKA DAR...

Wasanii wa Jahazi
 Imegundulika kwamba kwa sasa muziki wa taarabu umekuwa una soko zaidi mikoani ukilinganisha na Dar kama ilivyokuwa zamani. 

Uchunguzi uliofanywa na mtandao huu umebaini hilo haswa baada ya kuona katika shamrashamra za sikukuu ya IDD bendi nyingi zikitokomea mikoani na kuacha wapenzi wa Dar wakihaha kusaka burudani hiyo. 

Siku ya IDD tatu bendi ya Jahazi ilikuwa Morogoro, 
Bendi ya Kings ilikuwa Morogoro, 
Bendi ya 5 Stars ilikuwa Kibiti, 
Mashauzi walikuwa Songea. 
T Motto waliku Chanika.

Na Bendi zingine zilipumzika kabisa:-


East African Melody hawakuwa na show 
Supeshine hawakuwa na show 
Dar modern hawakuwa na show pia.
Coast Modern Taarab nao hawakuwa na show. 

Bendi ambayo ilikuwa na show siku ya IDDI tatu Dar nzima kwa upande wa Taarabu ni G5 Modern Taarabu pekee ambao walikuwa wanapiga pale Kalembo Bar maeneo ya Buguruni. 

Mpenzi mmoja wa Taarabu aitwae Jumanne Shabban aliuambia mtandao wa taarabuzetu.blogspot.com kwamba hawa viongozi wa hizi bendi hawakufanya vizuri kutuondolea burudani ya taarabu jijini. 

Bendi za Jahazi na Mashauzi bado zinaendelea na burudani za IDDI.

0 comments:

Post a Comment