TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Monday, August 19, 2013

UTENDAJI MBOVU NA USIO MAKINI NDIO CHANZO CHA KURUDISHA NYUMA MAENDELEO YA BENDI CHANGA ZA TAARABU NCHINI...


Huu ni uchunguzi uliofanywa na mtandao wa taarabuzetu.blogspot.com ya kuwa, hapa Tanzania kwa sasa unapoamua kuzungumzia bendi ya taarabu zinazofanya vizuri basi utataja tatu au nne tu, wakati kuna bendi za Taarabu takribani kumi na tano au kumi na sita hapa Dar es Salaam peke yake. 

Bendi zinazofanya vizuri ni:- 
Jahazi modern Taarabu, 
Mashauzi Modern Taarabu, 
5Star Modern Taarabu na wakongwe 
East African Melody tu basi!. 

Uchunguzi uliofanywa na mtandao huu makini kabisa umegundua kwamba takribani viongozi wote na wasanii wao wamekuwa ni watu wasiojiamini katika hii fani na ndio maana wanafikia hata kupiga nyimbo za kopi ambazo zinatamba katika bendi hizo ambazo wenyewe wanaziita kubwa!.

Kingine ni umakini wakati wakutengeneza nyimbo, madirector karibia wote waliopo katika hizi bendi ndogo ndogo wamekosa ubunifu, jinsi ya kubuni muziki wenyewe na mpangilio wa sauti kwa ujumla!, mbona mnaweza tu! hebu muwe mnajikubali na kamwe msitazame Jahazi au Mashauzi wamefanya nini. 

Hebu fanyeni kazi kwa uangalifu na umakini muone kama watu hawatowakubali!, kifurugobe alimdondokea kobe akaingiwa na hofu ya milele! acheni kukimbia kivuli chenu!. 

Wao waweze wana nini na ninyi mushindwe muna nini? 
PIGENI KAZI

0 comments:

Post a Comment