TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Tuesday, July 30, 2013

HEEH!! AISHA MASANJA WA T MOTO, KULIKONI TENA, MBONA UPO G5?

Aisha Masanja wa T. Moto
 Muimbaji Aisha Masanja ambae kiuhalisia yupo T MOTTO Modern Taarabu ameonekana akifanya mazoezi na bendi nyingine ya G5 Modern Taarabu, mwandishi wa habari hizi alipotaka kujua imekuwaje tena mpaka anafanya mazoezi na G5? au tayari yeye ni msanii wa bendi hiyo au anakula kotekote? alikataa na kusema kwamba yeye mpaka sasa bado ni msanii wa T MOTTO ila hapa G5 yupo yupo tu na kama atapewa wimbo kuimba yupo tayari ataimba, alipoulizwa je Mkurugenzi wako Amin Salmin anajua kama upo hapa G5? alisema hajui juu ya hilo. Mtandao wa taarabuzetu.blogspot.com unamuomba Aisha kuweka wazi!

0 comments:

Post a Comment