TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Tuesday, July 30, 2013

MATUKIO: KING'S WAKIREKODI NYIMBO ZAO TATU (3) LEO TAREHE 30/07/2013

Hanifa Maulid, Amina Mnyalu, Hanifa Juma wakiitikia wimbo wa Salha "No Discussion".
 Bendi ya King's Modern Taarabu, leo hii imefanikiwa kurekodi nyimbo zake tatu (3).
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ambaye alikuwepo kwenye Studio wakati wa kurekodi, Mkurugenzi wa Bendi Mr Hamis Majaliwa alizitaja nyimbo hizo ni:- 
1. Nimechoka na kashfa zenu - Muimbaji Aisha Othmani Vuvuzela, Kinanda - Omary Kisila na Maneno Keyboard, Solo - Mfaume Masuku na Bass - Silva Mundele.
2. No Discussion - Muimbaji Salha Abdallah. Kinanda - Mzaka Nundu na Ibrahim Kamongo, Solo - Mfaume Masuku, Bass - Silva Mundele.
3. Sikuumbwa Mnisimange iliyoimbwa na chipukizi Sophia Yahya. Kinanda - Mzaka Nundu na Ibrahim Kamongo, Solo na Bass - Silva Mundele.
Nyimbo zote zimerekodiwa katika Studio ya Sound Crafters chini ya Producer Enrico.  
 
Salha wa Hammer Q.
Mr Hamis Majaliwa alisema huo ni ujio mpya wa King's, na akaomba wapenzi wa Taarabu wajiandae kupata vibao vizuri na murua kabisa. 

King's ni miongoni mwa bendi zilizoingia katika shindano la Kilimanjaro Music Awards na ilishindania bendi bora ya Taarabu lakini haikubahatika kushinda, ila wamejipanga vyema kuleta ushindani na ameahidi lazima mwakani wafanye vyema zaidi..

Picha mbalimbali King's wakiwa wanarekodi...

Hassan Ally na Aisha Vuvuzela akipiga pozz...!!
Maneno na Omary Kisila wakipapasa Vinanda.
Wapiga Gitaa wa ukweli Mfaume Masuku na Silva Mundele.
Mwa4 wa EATV akiwa na wasanii wa King's ndani ya studio ya Sound Clafters.
Omary Kisilaakisababisha...
Silva Mundele akiwa na Mrisho Rajabu.
Sophia Yahya akiimba nyimbo ya "Sikuumbwa Mnisimange"...
Aisha Vuvuzela akiimba nyimbo ya "Nimechoka na Kashfa zenu".
Mfaume Masuku akikung'uta Gitaa la Solo...
Omary Kisila akifanya yake...


0 comments:

Post a Comment